Mwanariadha wa Uganda, Rebecca Cheptegei Afariki Dunia kwa Kuchomwa moto

 

Mwanariadha wa Uganda, Rebecca Cheptegei Afariki Dunia kwa Kuchomwa moto

Mwanariadha wa Uganda Rebecca Cheptegei amefariki Alhamisi alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali moja mjini Eldoret nchini Kenya kutokana na kushindwa kwa viungo vya mwili, Mkurugenzi wa Huduma za Kliniki katika kituo hicho Owen Menach amethibitisha.


Cheptegei ambaye alishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya mwaka huu alidaiwa kumwagiwa petroli na kuchomwa moto na mpenzi wake mjini Kitale Jumapili, na kusababisha mwili wake kuungua kwa asilimia 80 na hatimaye kufariki.


Shirikisho la Riadha la Uganda (UAF) pia limethibitisha kuaga dunia kwa Cheptegei katika chapisho kwenye akaunti yao rasmi ya X, na kutaka haki itendeke likisema "aliangukiwa na vurugu za nyumbani." "Tuna masikitiko makubwa kutangaza kifo cha mwanariadha wetu Rebecca Cheptegei mapema leo asubuhi, ambaye alihusika na dhuluma za nyumbani.


Kama shirikisho, tunalaani vitendo hivyo na tunaomba haki itendeke. Roho yake ipumzike kwa amani," lilisomeka chapisho hilo la wanariadha wa Uganda.



from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/3yDP9i8
via IFTTT

Post a Comment

Previous Post Next Post