Polisi Wafunguka Kuhusu Aliyetekwa Tegeta na Kukutwa Ameuawa Ununio....




Jeshi la Polisi limesema linaendelea na uchunguzi wa tukio la kusikitisha la mauaji ya Kiongozi wa CHADEMA, Ali Kibao na timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu kwenye timu ya awali ili kuhakikisha waliofanya mauaji haya wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime leo September 08,2024 imesema “Jeshi la Polisi linatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za kweli na za uhakika aziwasilishe kwa mujibu wa taratibu ili kusaidia kufanikisha kukamilika mapema kwa uchunguzi wa tukio hili la kusikitisha”

“Jana Septemba 7,2024 Jeshi la Polisi lilitoa taarifa juu ya Ally Mohamed Kibao kushushwa kutoka kwenye basi la Tashrif na kuchukuliwa na Watu ambao hawakuweza kutambulia na kwamba uchunguzi ulianza baada ya kupokelewa taarifa hiyo”

“Baada ya kutolewa taarifa za kuonekana mwili wa Mtu mwanaume ambaye hakuweza kutambulia kwa wakati huo ni mwili wa nani huko Ununio Jijini Dar es Salaam, utambulizi umefanyika kwa mujibu wa taratibu na kubainika ni mwili wa Ally Mohamed Kibao, aidha uchunguzi wa mwili wa marehemu (postmortem) umefanywa leo tarehe 08/09/2024 na Madaktari bingwa kwa kushirikisha Familia”


from UDAKU SPECIAL https://ift.tt/rR351YJ
via IFTTT

Post a Comment

Previous Post Next Post